Image
Image

Wachezaji wa soka ya wanawake wa Equatorial Guinea wadhaniwa wanaume

Bado Ile tabia ya wanawake kudhaniwa ni wanaume bado inaendelea michezoni na safari hii imemkuta mwanasoka wa Equatorial Guinea Genoveva.

Mbaya zaidi ni kwamba Genoveva alikutwa na kadhia hii toka kwa Waafrika wenziwe ambao ni viongozi wa mamlaka kuu za soka Afrika ambao walidhani binti huyu anadanganya kuhusu jinsia yake ya kike.

Mshambuliaji huyu wa timu ya taifa ya Equatorial Guinea alilazimishwa kuvua nguo na kukaguliwa ili kuthibitisha kuwa ni msichana na si mvulana kama ilivyokuwa inahofiwa na hii ni kutokana na nguvu ambazo anazo akiwa uwanjani na ubora alioonyesha.

Akizungumza na vyombo vya habari Genoveva alisema alidhani uthibitisho wa jinsia hufanywa hospitalini lakini cha kushangaza ni kwamba alilazimishwa kuvua nguo na kukaguliwa jambo ambalo anakiri kuwa lilimsababishia fedheha na hasira.

Kashfa hii ilianzishwa kwenye muichuano ya kombe la mataifa ya Afrika kwa kina mama ambapo viongozi wa Ghana, Nigeria na Afrika Kusini walizusha hoja kuwa wachezaji watatu wa Equatorial Guinea ni wanaume na si wanawake.

 Hofu hii iliondolewa baada ya wachezaji hawa kukaguliwa na kugundulika kuwa ni wanawake halisi

 


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment