Image
Image

News Alert:Dr.Bilal amesema njia pekee ya kupambana na rushwa nchini na barani Afrika ni kushirikisha asasi za kiraia.


Makamu wa rais Dr Mohammed Gharibu bilal amesema njia pekee ya kupambana na rushwa nchini na barani afrika kwa ujumla ni kwa serikali kuzishirikisha na kuwezesha asasi za kiraia katika kupiga vita utoaji na upokeaji rushwa kwani ndizo zinazowatetea wanyonge badala ya kutegemea taasisi moja pekeee.
Dr. Bilal ameyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati akifungua mkutano wa tano wa wakuu wataasisi za kupambana na rushwa kwa nchi 54 wanachama wa jumuiya ya madola ambapo amebainisha kuwa bila usafi wa viongozi wa kisiasa na watumishi wa umma katika kukataa

Rushwa tatizo la hilo bado litaendelea kuwa changamoto katika kufikia malengo ya maendeleo.

Jumuiya ya afrika mashariki ikitanguliwa na rwanda waziri wa nchi ofisi ya rais utawala bora Kapteni mstaafu George Mkuchika amekiri kuwa tatizo la rushwa hasa kwa viongozi wa nafasi za juu serikali inatia doa utawala bora nchini na kusema kuwa mapambano hayo hasa kwa watumishi wa umma yanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukuwaji wa technologia.

Kwa upande wake mkurugenzi wa tasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini takukuru Dr. Edward Hosea amesema kuwa miongoni mwa maeneo sugu ya utoaji na upokeaji rushwa ni katika kipindi cha uchaguzi na hapa anaeleza jinsi Takukuru ilivyojiandaa kupambana na rushwa katika uchaguzi mkuu wa mwezi October mwaka huu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment