Image
Image

News Alert:Serikali yatakiwa kuongeza nguvu ili kukomesha mauaji ya Albino.


Serikali imetakiwa  kuhakisha  kuwa  inaongeza  nguvu  katika  kuhakisha  kuwa  mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi  yanakomeshwa  kwani  tatizo  hilo limekuwepo kwa muda  mrefu   lakini  ufumbuzi  wake  umebaki  kuwa  kitendawili  na  hivyo kuwa ni  aibu  na  fedheha kubwa kwa taifa. 

Hayo   yamesemwa   katika hotuba  ya   msemaji  wa kambi  ya  upinzani Bungeni  wa wizara  ya maendeleo ya jamii  jinsia na watoto Mh. Salum  Khalfan  Barwany  iliyosomwa  na Mh. Esther matiku ambapo  amesema  sasa  suala  la  mauji  ya  alibino  limekuwa tishio  kubwa.

Kwa upande  wa kamati  ya kudumu ya   maaendeleo  ya  jamii  imesema kuwa sababu kubwa ya mambo  mengi  kushindwa  kwenda  kama  inavyotakiwa ni serikli kutenga  fedha  katika wizara  zake  hasa  ya  maendeleo  ya  jamii  na  kutokuzikupeleka  na hata ikipeleka haipeleki  kwa wakati.

Awali katika kikao hicho Mh.Sophia  Simba waziri  wa wizara ya maendeleo ya jamii jinsi na watoto  na Mh. Gaudentia Kabaka  waziri wa kazi na ajira waliwasilisha bajetia za wizara zao ambapo kila mtu alijinadi ni kwa namna gani atakavyotumia fedha hizo. 

Wakichangia bajeti  hizo baadhi ya wabunge wamesema bado tatizo la ajira ni kubwa nchini  ukilinganisha  na  ahadi  zinazotolewa  za  ajira na baadhi yao wakitaka  vyuo  vya  maendeleo ya jamii vitumike ipasavyo ili kusaidia  kupatikana kwa wataalamu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment