Msaada huo wa madawati umeelezwa kuwa utasaidia kuimarisha
kiwango cha elimu na kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wa shule za msingi.
Akizungumza wakati wa zoezi la kukabidhi madawati
hayo mkurugenzi wa kampuni ya Tigo kanda ya ziwa Bw.Ally Maswanya amesema
kampuni yake inatambua umuhimu wa elimu kwa watanzania na kampuni imeamua
kurudisha sehemu ya faida yake kwa jamii katika upande wa elimu ili kuendelea
kuimarisha sekta hiyo.
Hata hivyo naye aimu katibu tawala wa mkoa wa
shinyanga Bw.Projectus Rubwanzibwa amesema msaada huo utasaidia kupunguza
tatizo sugu la madawati linaoukabili mkoa wa shinyanga kwa muda mrefu na kukuza
kiwango cha elimu huku baadhi ya wanafunzi wa shule zilizopata mzaada huo
wakionyesha furaha waliyoipata na kwa upande mwingine wakiahidi kufanya vizuri
katika masomo yao.


0 comments:
Post a Comment