Wakati huohuo, rais Pierre
Nkurunziza amesaini amri ya kuitisha mkutano maalumu wa mabaraza mawili ya
bunge la nchi hiyo Mei 20 na 21, bila kueleza sababu ya kuitisha mkutano huo.
Habari nyingine zinasema
Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limeihimiza jumuiya ya
kimataifa kutoa msaada kutokana na idadi ya wakimbizi kutoka Burundi
walioambukizwa ugonjwa wa kipindupindu kuongezeka hadi kufikia zaidi ya 1,000.
Mjumbe maalumu wa shirika
hilo nchini Tanzania Joyce Mends-Cole amesema hali ni mbaya. Mpaka sasa
wakimbizi 17 wa Burundi wamefariki kutokana na maambukizi ya ugonjwa wa
kipindupindu.


0 comments:
Post a Comment