Serikali imewaomba radhi
wanafunzi wa vyuo vikuu kwa hatua walizopitia kutokana na fedha za kujikimu
kuchelewa na kwamba fedha zimeshatoka hazina huku ikizitaka taasisi zinakopita
fedha hizo kuhakikisha zinawafikia wanafunzi leo leo.
Naibu waziri wa fedha Mh. Mwigulu Nchemba amelazimika kutoa ufafanuzi huo juu ya madai ya wanafunzi wa vyuo vikuu yaliyosababisha jana wagome, baada ya Mh .Esther Bulaya mbunge wa viti maalum kuomba muongozo wa mwenyekiti kuhusiana na suala hilo Bungeni mjini Dodoma.
Naibu waziri wa fedha Mh. Mwigulu Nchemba amelazimika kutoa ufafanuzi huo juu ya madai ya wanafunzi wa vyuo vikuu yaliyosababisha jana wagome, baada ya Mh .Esther Bulaya mbunge wa viti maalum kuomba muongozo wa mwenyekiti kuhusiana na suala hilo Bungeni mjini Dodoma.
Katika viwanja vya chuo kikuu
jijini Dar es Salaam walisema endapo serikali haitasikia kilio chao na
kukipatia ufumbuzi basi wataendelea na mgomo hadi fedha zitakpoingia kwenye
akaunti zao.
Kwa upande wake makamu mkuu
wa chuo kikuu cha Dar es Salaam Prof. Rwekaza Mukandara pamoja na kukiri madai
ya wanafunzi elfu saba kati ya zaidi ya elfu kumi wanaofadhiliwa na serikali
kupitia bodi ya mikopo kucheleweshewa fedha zao kuwa ya msingi amesema tayari
amezungumza na bodi ya mikopo ambao wamemwahidi kuleta fedha zao haraka
iwezekanavyo na kuwaomba wanafunzi kurejea madarasani kuendelea na masomo.
Wakati huohuo takribani
wanafunzi 400 wa chuo kikuu cha Mt. Josephu cha Mbezi jijini Dar es Salaam
mwaka wa kwanza wamesimamishwa masomo kwa muda usiojulikana baada ya kugoma
kuingia madarasani wakidai fedha za kujikim kutoka bodi ya mikopo tangu mwezi
Desemba mwaka jana hadi sasa wakieleza kuishindwa kuendesha maisha yao ya shule
na kuhimili mazingira ya kupangha nyumba mitaani.
Katika taarifa ya kusimamisha
wanafunzi hao iliyotolewa na makamu mkuu wa chuo cha Mt.Josephu Bw.Loyola
Proteep aliyeambatana na mkuu wa wanafunzi maarufu kama Dean anakiri madai ya
wanafunzi hao kuwa ya msingi na kuongeza kuwa waliwaomba utulivu na kuingia
Madarasani wakati wakifuatilia madai yao bodi ya mikopo bila ya mafanikio na
uongozi kuchukua uamuzi wa kuwasimamisha wanafunzi wote wa mwaka wa kwanza hadi
vikao vya bodi vitakapoamua vinginevyo.
Kauli ya Mwigulu Nchemba Bungeni leo ndiyo hii.
Kauli ya Mwigulu Nchemba Bungeni leo ndiyo hii.


0 comments:
Post a Comment