Wakati mchakato huo ukisubiri mashabiki kuamua
msanii yupi aingie katika kipengele kipi, wasanii wengi watakuwa matumbo joto
kwa kile kinachoelezwa kwamba KTMA sasa zimekubalika zaidi kwao na mashabiki wa
muziki.
Hata hivyo, msimu huo unatojawa kuwa wenye neema kwa
wasanii, unazua maswali mengi vichwani mwa wasanii na mashabiki wao moja
likiwa; ni nani atavunja rekodi iliyowekwa na mwanamuziki Diamond Platnumz
mwaka jana?
Mbali na Diamond kuvunja rekodi msimu uliopita,
Bendi ya muziki wa dansi ya Mashujaa pia iliwahi kunyakua tuzo tano mwaka 2013,
huku wasanii, Kala Jeremiah na Ommy Dimpoz wakinyakua tuzo tatu kila mmoja.
Shabiki wa muziki wa kizazi kipya na mfanyabiashara
katika Soko la Kariakoo, Omary Shaban alisema ushindani kwa mwaka huu utakuwa
mkubwa kwa tuzo hizo, hasa ikizingatiwa uwepo wa wanamuziki wengi wazuri
waliofanya kazi tofauti, zenye ubora na viwango vya juu.
“Mwaka jana Diamond Platnumz alinyakua tuzo nyingi
kwa kuwa alijaribu kufanya kitu tofauti, lakini alichokifanya na wengine
wamefanya. Hivyo, ana ushindani mkubwa, pia Alikiba ambaye alikuwa kimya
amerudi. Hawa wawili ni washindani wakubwa, hivyo video zao zitalumbana sana,
yaani tunasubiri kumjua mkali nani,” anasema Shaban.
Mshabiki mwingine, Ally Elly wa Dar es Salaam
alisema ni vyema kusiwepo ubabaishaji ili wapatikane washindani na washindi
halisi wa tuzo hizo kwa mwaka huu.
Mchakato
utakavyokuwa
Waandaji wa mashindani hayo walisema kuwa kwa mwaka
huu kuna ongezeko la baadhi ya mambo, lengo likiwa ni kuboresha utoaji wa tuzo
hizo na kuwapa fursa Watanzania kupendekeza wasanii watakaowania tuzo hizo kwa
kuwapigia kura waingie kwenye kinyang’anyiro kwa njia tatu kuu.


0 comments:
Post a Comment