Image
Image

Kili Music Award 2015?.


Msimu wa utoaji tuzo kwa wasanii wa muziki Tanzania wanaofanya vizuri umewadia huku mchakato wa awali wa mchanganuo wa tuzo hizo za Kili Tanzania Music Awards 2015 (KTMA) ukianza rasmi wiki hii.
Wakati mchakato huo ukisubiri mashabiki kuamua msanii yupi aingie katika kipengele kipi, wasanii wengi watakuwa matumbo joto kwa kile kinachoelezwa kwamba KTMA sasa zimekubalika zaidi kwao na mashabiki wa muziki.
Hata hivyo, msimu huo unatojawa kuwa wenye neema kwa wasanii, unazua maswali mengi vichwani mwa wasanii na mashabiki wao moja likiwa; ni nani atavunja rekodi iliyowekwa na mwanamuziki Diamond Platnumz mwaka jana?
Mbali na Diamond kuvunja rekodi msimu uliopita, Bendi ya muziki wa dansi ya Mashujaa pia iliwahi kunyakua tuzo tano mwaka 2013, huku wasanii, Kala Jeremiah na Ommy Dimpoz wakinyakua tuzo tatu kila mmoja.
Shabiki wa muziki wa kizazi kipya na mfanyabiashara katika Soko la Kariakoo, Omary Shaban alisema ushindani kwa mwaka huu utakuwa mkubwa kwa tuzo hizo, hasa ikizingatiwa uwepo wa wanamuziki wengi wazuri waliofanya kazi tofauti, zenye ubora na viwango vya juu.
“Mwaka jana Diamond Platnumz alinyakua tuzo nyingi kwa kuwa alijaribu kufanya kitu tofauti, lakini alichokifanya na wengine wamefanya. Hivyo, ana ushindani mkubwa, pia Alikiba ambaye alikuwa kimya amerudi. Hawa wawili ni washindani wakubwa, hivyo video zao zitalumbana sana, yaani tunasubiri kumjua mkali nani,” anasema Shaban.
Mshabiki mwingine, Ally Elly wa Dar es Salaam alisema ni vyema kusiwepo ubabaishaji ili wapatikane washindani na washindi halisi wa tuzo hizo kwa mwaka huu.
Mchakato utakavyokuwa
Waandaji wa mashindani hayo walisema kuwa kwa mwaka huu kuna ongezeko la baadhi ya mambo, lengo likiwa ni kuboresha utoaji wa tuzo hizo na kuwapa fursa Watanzania kupendekeza wasanii watakaowania tuzo hizo kwa kuwapigia kura waingie kwenye kinyang’anyiro kwa njia tatu kuu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment