Image
Image

KIUNGO Msierra Leone, Lansana Kamara, anatarajiwa kusaini mkataba wakati wowote kuanzia keshokutwa Jumatatu.


KIUNGO Msierra Leone, Lansana Kamara, anatarajiwa kusaini mkataba wakati wowote kuanzia keshokutwa Jumatatu ili kuitumikia Yanga, lakini wakati akipokea taarifa hizo njema amechimba mkwara mzito na kuwahakikishia mashabiki wa timu hiyo kuwa atawafanyia kazi nzito.
Mchezaji huyo anayeichezea pia timu yake ya taifa, amewaambia Yanga kwamba hajaja nchini kuuza sura, bali kufanya kazi na  ameangalia  staili ya uchezaji ya Yanga kisha akasema: “Mbona freshi tu hapa nitapiga kazi sana, mimi ni jembe.”
Naye wakala wake, Gibby Kalule, alisema Kamara ni mchezaji mzuri lakini Yanga  ndio yenye maamuzi ya mwisho kama kumsajili au la, naye akasisitiza jamaa ni jembe.
Uongozi wa Yanga umemhakikishia maisha kiungo huyo mrefu kuwa ukimwambia kuanzia Jumatatu kila kitu kitakuwa sawa huku  Mwanaspoti ikifahamu klabu hiyo inataka kujihakikishia juu ya idadi halisi ya wachezaji wa kigeni watakaoruhusiwa kusajili msimu ujao.
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kesho Jumapili litakuwa na kikao kizito kitakachoamua mabadiliko ya idadi ya wachezaji wa kigeni wanaopendekezwa kuzitumikia klabu shiriki za Ligi Kuu Bara kutoka watano wa sasa hadi kuwa kumi.
Akizungumza na Mwanaspoti, Kamara alisema anasubiri kwa hamu lolote ambalo Yanga watataka alifanye chini ya kocha Hans Pluijm.
Kamara alisema yuko tayari kufanyiwa majaribio yoyote na Pluijm katika kupima ufanisi wake wa kucheza nafasi ya kiungo mkabaji na hata mchezeshaji ambapo baada ya kuona soka la Yanga kwa sasa amejihakikishia nafasi katika kikosi hicho.
“Nimekuja kufanya kazi hapa, ndiyo maana unaona nafanya mazoezi yangu binafsi kujiweka sawa, sitaki kuharibu ubora wangu, najiamini kwamba kazi naiweza nitawafanyia kazi Yanga ngoja tumalizane,” alisema Kamara ambaye wakati wowote anaweza kupata taarifa za kuitwa baba kwa mara ya kwanza.
Yanga kupitia Katibu wake, Dk. Jonas Tiboroha aliwahi kuliambia Mwanaspoti kuwa wamevutiwa na umbo la mchezaji huyo, pia hata mikanda yake ya video lakini akataka wapewe muda.
“Tupeni muda kidogo tufanye majukumu yetu kwa kina,” alisema Tiboroha.
Endapo Kamara atafanikiwa kusajiliwa na Yanga ni wazi sasa safu ya kiungo mkabaji anayomudu kuichezea inaweza kuwa na ushindani mkali.
Hiyo ni kutokana na ukweli kuwa tayari viungo Salum Telela na kinda Said Juma Makapu wametangulia kujizolea sifa katika nafasi hiyo katika mechi mbalimbali za Yanga.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment