Image
Image

LIGI KUU ENGLAND 2015/16: Je, msimu ujao mabingwa ni Arsenal au Manchester United?


London, England

Baada ya wiki iliyopita Manchester United na Arsenal kutoka sare ya bao 1-1 kwenye Uwanja wa Old Trafford, timu hizi zilionyesha kwamba haziwezi kuitoa Manchester City katika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu England huku zikiwa zimeishakubali Chelsea kuwa bingwa.

Jarida hili la Spoti Mikiki linazichambua Manchester United na Arsenal kama zinaweza kuizidi Chelsea msimu ujao na kutwaa ubingwa wa 2015/16.

Je, zina vikosi vitakavyowawezesha kutwaa ubingwa au zinasajili wachezaji gani ili ziweze kutwaa ubingwa?

Arsenal

Miezi kadhaa iliyopita nyota wa zamani wa Arsenal, Thierry Henry aliwahi kukikosoa kikosi cha Arsenal na kupendekeza kwamba kinatakiwa kufanya usajili haraka, Henry alikuwa na pointi. Arsenal inatakiwa kuboresha idara ya golini. Kipa

Wojciech Szczesny (ambaye alianza msimu huu akiwa chaguo la kwanza) na kipa David Ospina (aliyemalizia msimu) wote walionyesha udhaifu kuliko makipa wengine wa timu zilizo katika nafasi za juu katika msimu wa Ligi Kuu England. Katika kiungo, kiungo mkabaji Francis Coquelin alijitahidi msimu huu, lakini Arsenal wakimchukua na Morgan Schneiderlin wa Southampton watafanya vizuri. Katika safu ya ushambuliaji mbadala wa Olivier Giroud unahitajika. Ni kazi kupata washambuliaji bora, lakini Arsenal haina jinsi inatakiwa kusajili. Danny Welbeck alijitahidi, lakini aliumia. Arsenal ipo vizuri katika safu ya ulinzi wa kati na mwanzoni mwa mwaka huu ilimsajili beki Gabriel Paulista.

Manchester United

Usawa kwa wachezaji katika kila nafasi ndiyo falsafa ya kocha Louis van Gaal wa Manchester United.

“Haijalishi una kikosi kikubwa kiasi gani au idadi kubwa ya namba ya wachezaji, kinachohitajika ni usawa wa wachezaji katika kila nafasi, ninapokuwa na wachezaji wawili wenye uwezo wa juu katika kila nafasi basi huwa nina furaha,”alisema Van Gaal.

Hata hivyo tishio kubwa kwa Van Gaal ni taarifa kuwa kipa wake David de Gea anaoondoka na kujiunga na Real Madrid. Ni taabu hivi sasa kupata kipa makipa wenye ubora wa juu duniani. Hata hivyo Van Gaal akipata saini ya kipa wa Tottenham Hotspur, Hugo Lloris atakuwa amelamba dume. Hata hivyo kocha huyu anatakiwa kusajili zaidi, anatakiwa kusajili kiungo mwenye ubora wa juu kama Paul Pogba wa Juventus, beki wa kulia kama Seamus Coleman wa Everton, beki wa kati kama Mats Hummels wa Borussia Dortmund na washambuliaji kama Harry Kane wa Tottenham Hotspur na Gareth Bale wa Real Madrid.

Je, makocha Arsene Wenger wa Arsenal na Van Gaal wa Manchester United wafanye nini kubadilisha vikosi vyao ili watwae ubingwa msimu ujao?
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment