Wakizungumza na Tambarare Halisi
wakati wakiwasilisha kilio chao kwa lengo la kutafutiwa ufumbuzi na viongozi
wanaohusika pindi watakapo iona habari hiyo vijana hao ambao wametoka maeneo ya
kawe,tangibovu na maeneo jirani wamesema wameunganisha nguvu ili kupinga
vitendo wanavyo fanyiwa na vikundi hivyo kwani imekuwa nikama desturi hali
ambayo wamekuwa wakinyanyasika na huku wakiwa na familia zinazo wategemea.
Wamesema kuwa wao kama waendesha
bodaboda hawana ugomvi wa aina yeyote na askari wa usalama barabarani kwa kuwa
endapo mtu atakuwa kakiuka sheria za usalama bara barani basi watapigwa faini
inayo landanda na kosa lenyewe tofauti na vikundi ambavyo havina sare wala
vitambulisho vinavyoibuka kwa lengo la kujitafutia maslahi binafsi katika
mgongo wao bila hata huruma ya aina yeyote.
Makundi hayo yamekuwa mara kadhaa
yakiwavizia wakati wakiwa kwenye foleni na hivyo kuwanyang”anya funguo wakiwataka
wawapatie kiasi cha fedha wanazo taka wao,hali ambayo waendesha bodaboda
wanadai kuwa wanaendesha pikipiki hizo kimachale kwani wanapo waona wanakimbia
ndipo wakati mwingine hujikuta wakipata ajali zisizo na sababu kwa kukwepa
kulipa fedha ambazo hazijulikani zina kwenda wapi.
Kufuatia malalamiko hayo ya
waendesha Bodaboda Tambarare ikafanikiwa kuzungumza na mkuu wa kikosi cha
usalama barabarani mkoa wa kiondondoni kamanda Awadhi Haji kwa lengo la kutaka
kufahamu kwamba je malalamiko haya wanayajua ama la?. Na kama wanayajua zipi juhudi
walizofanya kutatua hili?.
Kamanda Awadhi amesema kuwa
kikosi chake kipo safi katika kutekeleza majukumu kwa mujibu wa sheria na hivyo
askari wake wakiwa wamevalia sare kila wawapo sehemu ya kazi na hivyokusema
kuwa”Kwa malalamiko haya kuna kunasababu na haja ya madereva kufika ofisini
kwangu na kutoa ushirikiano mzuri ili kuweza kukomesha makundi ambayo
yanalichafulia heshima jeshi la polisi kwa kupokea rushwa kinyume na taratibu
na hivyo sheria kufuata mkondo wake.
Bwana.Kalos Mbwalo ni
mwakilishi/mwenyekiti asiye rasmi aliyechaguliwa na wenzie ili kuweza kufikisha
kiliochao,ambapo amesema”Sisi tuliofika hapa niwachache ila tunawakilisha
wenzetu wengine ambao wapo maeneo mbali mbali ya mjii huu wa Dar es Salaam
wakipatwa na kadhia hii ya kutoa rushwa pasipo kujulikana fedha zina kwenda
wapi”Alisema Mbwalo.
Amesema wao kipo kitu wanacho
kishangaa mno hasa katika taifa hili ambalo hiki ni kipindi cha uchaguzi kwa
namna kunavyoonekana kuwepo kama na ubaguzi kutokana na kwamba ingawa serikali
imekataza pikipiki hizo kuingia mjini lakini wanashangaa kwamba mbona wapo
waendesha bodaboda mjini na wanaingia maeneo mengine kupeleka abiria sasa Je
mbona wao wakiingia mjini hukumbana na vikwazo vingi,kwani hizo piki piki zina
mkono wa watu wakubwa(Vigogo)ama tafsiri yake nini haswa jambo hilo linawapa
kigugumizi kikubwa.
Kutokana na changamoto
wanazokutana nazo hizo wameelekeza kilio chao kwa kikosi cha usalama barabarani
pamoja serikali yake kwa ujumla kuangalia namna ya kuwasaidia kwani kazi
wanayoifanya ni yakujiingizia kipato pamoja na familia zao,na kutokana na ajira
kuwa ngumu wamejiajiri wenyewe lakini wachache wanawanyonya kwa hata kidogo
wanacho kipata jambo ambalo linawaumiza kwa kiasi kikubwa.
Wanadai kuwa katika kazi hiyo ya
kuendesha boda boda kwa wao usalama ni hafifu kufuatia siku za nyuma walikuwa
wana kabwa na kuuawa na pikipiki zao kuibiwa,na wanaofanya shughuli hiyo ni
watu wanao tumia magari ya NOAH ambayo wao wenyewe wanayaogopa kwani yamekuwa
yakifanya shughuli za kihalifu,kwani wanapo tekeleza jaribio la wizi kwa
waendesha boda boda huwapiga na kutupwa nje na pikipiki kupakiwa kwenye gari
hiyo na kuondoka nayo hivyo jeshi liangalie kwa umakini wasidhani bodaboda tu
ndio wahalifu mbinu za uhalifu zimebadilika.
Hata hivyo wamesema kwamba
kutokana na matatizo hayo sasa wapo makini kuangalia kiongozi atakaye faa na
kutatua matatizo yao na huyo ndiye watakaye mpatia na kumpigia kura hapo Octoba
mwaka huu katika uchaguzi mkuu.


0 comments:
Post a Comment