Image
Image

Al-Shabaab wakanusha vikali madai ya rais wa Burundi Piere Nkurunzinza kwamba wana mpango wa kushambulia Burundi.


Kikundi cha al-Shabaab cha Somalia kimekanusha madai ya Rais PIERRE NKURUNZIZA wa Burundi kwamba kinapanga kushambulia nchi yake na kudai hicho kilikuwa kihoro cha mgogoro wa kisiasa wa nchi yake.
Bwana NKURUNZIZA ambaye amekabiliwa na wiki za maandamano kupinga uamuzi wake wa kugombea muhula wa tatu na jaribio la mpinduzi alijitokeza hadharani kwa mara ya kwanza katika mji mkuu wa nchi hiyo, Bujumbura hapo jana.
Lakini katika kauli yake hakugusa mambo ya maandamano na jaribio la mapinduzi na badala yake alichosema ni kwamba mawazo yake zaidi yako kwenye tishio la kikundi cha al-Shabaab kwa nchi yake.
Burundi ni miongoni nchi za wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika huko Somalia ambazo zimekuwa zinalengwa kwa mashambulio na kikundi cha al-Shabaab.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment