Image
Image

News Alert:Serikali kufanya operesheni maalumu kuwakamata waganga wa jadi wanaopiga ramli.


Serikali  imesema  itaendelea kufanya  operesheni  maalum na za mara  kwa mara  ili kuwakamata waganga wa jadi  wanaopiga ramli chonganishi  kwani wamekuwa  ni kichocheo kikubwa  kwa  kudai kwamba  kiungo  cha  Alibino kina bahati  ya  utajiri.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri  wa Ma m bo ya Ndani  ya nchi ,PERE IRA  AME SILIMA alipokuwa   akijibu swali la   Mbunge  PHILIPA MTURANO   aliyetaka kujua   mpaka sasa  ni watu wangapi wanashikiliwa  na kuthibitishwa na mahakama  kuwa ndiyo  wauaji  na imefanya nini.
Naibu Waziri  amesema  Serikali kupitia  jeshi  la polisi imekuwa  ikichukua  hatua  za makusudi  kukomesha mauaji  hayo  ikiwa ni pamojaa na  kuwasaka  kuwakamata  na kuwafkisha   mahakamani  watuhumiwa  husika.
Amesema  mpaka   sasa  watu 15  wa muaji  ya Albino  wamekamatwa  na kufikishwa  mahakamani   na  kuhukumiwa   kunyongwa  hadi  kufa .
Aidha  serikali kupitia  jeshi la polisi  kwa kutumia  falsafa  ya  polisi  jamii  inafanya  kila  jitihada   ya  kutoa  elimu  kwa jamii  ili kuweka  ufahamu  juu ya madhara   ya  vitendo  vya  mauaji   vinavyofanywa  na   baadhi ya  watu  kwa msukumo  wa  imani  potofu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment