Image
Image

UNHCR limewataka wakazi wa mikoa ya Kagera na Kigoma kuto wahifadhi majumbani wakimbizi.


Shirika linalohudumia  wakimbizi UNHCR  limewataka wakazi  wa mikoa ya Kagera na Kigoma kuto wahifadhi  majumbani wakimbizi wanaoingia nchini bila kufuata taratibu zinazo husika badala yake watoe taarifa kwenye mamlaka husika  ili kujiepusha na madhara ambayo yanaweza kujitokeza dhidi yao.
Mshauri wa operesheni na sheria za wakimbiz  UNHCR  Profesa Bonaventure  Rutinwa amesema hayo wakati akitoa semina kwa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Kagera ambapo amewataka wakazi wa mkoa wa kagera na kigoma kutoa taarifa haraka pindi wanapo ona dalili za wakimbizi wanaoingia nchini bila ratibu maalumu  nakuwataka wasiwahifadhi wakimbizi majumbani mwao badala yake watoe taarifa kwenye mamlaka husika  kwaajili ya kuepuka madhara mabalimbali ikiwemo maradhi  ambayo yaneweza kujitokeza.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalam  ambae pia ni mkuu wa mkoa wa kagera John Mongera amesema serikali imelipokea hilo na italishughulikia kwa kutoa elimu kwa wananchi wa mkoa huo juu ya madhara ya kuwapokea na kuhifadhi  wakimbizi  bila utaratibu na kuongeza wakimbizi wanapokelewa kwa kufuata kanununi na sheria zilizoweka na umoja wa mataifa nakwamba serikali ya mkoa wa kagera imekwisha pokea wakimbizi miasita  ambao sasa wamesafirishwa na kupoelekwa katika kambizi za wakimbizi zilizopo mkoani kigoma.
Hali hiyo imejitokeza mara baada ya vuguvugu la machafuko linaloendelea huko nchini burundi  ambapo sasa kumekuwa na wimbi la wakimbizi wanaoingia nchini bila utaratibu  ambapo shirika la kuhudumia wakimbizi UNHCR  limelazimika kukutana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Kagera kwaajili ya kujadili namna ya kukabiliana na tatizo hilo.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment