Image
Image

News Alert:Wauguzi zaidi ya 400 katika hospitali ya rufaa Bugando wamuomba mkurugenzi kuwaongezea malipo ya zamu za usiku.


Wauguzi zaidi ya 400 katika hospitali ya rufaa Bugando jijini Mwanza wamemuomba mkurugenzi mkuu wa hospitali hiyo Prof. Dk. Kien Mteta kuwaongezea malipo ya zamu za usiku kutoka shilingi 2000 wanazolipwa hivi sasa hadi kufikia shilingi 15,000 ili kuwapa  motisha ya kazi na pia kumudu gharama za maisha kutokana na kufanya kazi kwa zaidi ya saa 14.

Katibu wa chama cha wauguzi tanzania ( TANNA ) tawi la hospitali ya rufaa Bugando  Lydia Chuwa  ametoa ombi hilo wakati akisoma risala ya siku ya wauguzi duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka kwa ajili ya kukumbuka siku aliyozaliwa muasisi wa taaluma ya uuguzi duniani Bi. Florence  Nightingali ambapo kaulimbiu ya mwaka huu inasema wauguzi ni nguvu ya mabadiliko, huduma bora gharama nafuu.

Akizungumza na wauguzi hao mkurugenzi mkuu wa hospitali ya rufaa bugando Prof. Dk. Kien Mteta amewataka wauguzi kuhakikisha wanatoa huduma nzuri kwa wagonjwa ili ziweze kuleta matokeo chanya katika taswira ya uuguzi, ambapo pia amewashauri kujiendeleza kimasomo na kuzingatia maadili katika kutoa huduma kwa wateja na hivyo kuwa nguvu ya mabadiliko na raslimali muhimu ya afya.

Baadhi ya wauguzi wamesema wataendelea kuzingatia viapo vyao walivyoviapa wakati wanahitimu taaluma ya uuguzi licha ya kufanya kazi katika mazingira yenye changamoto nyingi.

Kisha ukawadia wakati wa mkurugenzi wa huduma za uuguzi katika hospitali hiyo Bi. Mashauri kuwaongoza wauguzi hao 434 katika tendo la kuwasha mishumaa na kurudia kiapo chao.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment