Image
Image

News Alert:Kupinduliwa serikali ya Nkurunziza wakuu wa EAC walaani*Nkurunziza ashindwa kuhudhuria mkutano wa EAC Arudi Burundi.



Wakuu wa nchi  za jumuiya ya afrika  mashirika wamelaani jaribio la mapinduzi  yaliyotaka kufanyika nchini burundi huku wakitaka utawala wa sheria kwa kuheshimu katiba na makubaliano ya arusha  pamoja na kusogezwa mbele.

Akisoma maazimio ya mkutano huo mwenyekiti wa jumuiya hiyo Rais Jakaya Kikwete amesema wanatambua hali ya kisasa iliyotokea burundi na hivyo wanasisitiza makubaliano ya Arusha yaheshimiwe.

Mkutano huo umekubaliana kwa pamoja uchaguzi wa burundi usogezwe mbele hadi hali ya siasa itakapotengemaa.

Tofauti na matarajio ya wengi Rais Pierre Nkurunziza hakuweza kuhudhuria mkutano huo licha yakuwepo taarifa kuwa aliwasili jijini Dar es Salaam.


Hata hivyo mkutano huo hakuweza kufanyika katika utaratibu ambao umepangwa kufuatia kuwepo kwa taarifa ya kuwepo mapinduzi nchini Burundi ambapo taarifa hizo zimeibua taharuki na wasiwasi miongoni mwa washiriki wa mkutano huo  wakiwemo viongozi kutoka nchi wanachama.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment