Image
Image

Wakimbizi wa Kisomali warejea kutoka Yemen.


Hali mbaya ya ukosefu wa amani nchini Yemen iliyosababishwa na mashambulio ya kinyama ya Saudi Arabia katika nchi hiyo, yamepelekea maelfu ya wakimbizi wa Kisomali waliokuwa nchini humo kurejea kwao.
Nicholas Kay, mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia ametangaza kuwa, wakimbizi elfu saba wa Somalia waliokuwa nchini Yemen wamerejea nchini kwao baada ya usalama nchini Yemen kuzidi kuwa mbaya. 
Nicholas Kay amesema hayo katika hotuba yake kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kubainisha kwamba, kuna haja ya kuweko usimamizi wa karibu kwa wakimbizi hao wanaorejea nchini Somalia. 
Aidha amesema, kuna ulazima wa kuchukuliwa hatua za kukabiliana na tishio la kundi la kigaidi la al-Shabab. Ripoti za Umoja wa Mataifa zinaonesha kuwa, kuna wakimbizi laki mbili na nusu wa Somalia nchini Yemen.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment