Image
Image

Breaking News:Ajali ya Coaster na Lori yaua 23 na kujeruhi 34 katika eneo la KINYANABO,Mafinga.



Watu 23 wamekufa na wengine 34 wamejeruhiwa, wanne kati yao hali zao ni mbaya,kutokana na ajali iliyotokea katika eneo la Kinyalamambo, Mafinga Mkoani iliyohusisha basi dogo aina ya Coaster  na lori la mizigo.

Magari hayo yaligongana kwenye barabara kuu ya Iringa-Njombe na chanzo cha ajali hiyo ni mwendo-kasi.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, PUDENCIANA PROTAS  amesema baso hilo lilikuwalikitokea Iringa kwenda Njombe na kwamba majeruhi 30 wamefahamika kwa vile wanaweza kuzungumza na hali zao zinaendelea vizuri.

Amesema miongoni mwa waliokufa ni dereva wa lori  na wengine 22 ni kutoka kwenye basi na miili imehifadhiwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Mafinga na maiti 12 wametambuliwa na waliobaki hawajatambuliwa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment