Image
Image

ICC yaamua kesi ya mbabe wa kivita BOSCO NTAGANDA isikilizwe The Hague, Uholanzi.


Majaji wa Mahakama ya Uhalifu ya Kimataifa ya ICC wameamua kesi ya mbabe wa kivita wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo BOSCO NTAGANDA isikilizwe makao makuu ya mahakama hiyo iliyoko The Hague, Uholanzi.
Awali majaji wengine walitaka sehemu ya kesi hiyo isikilizwe mji wa Bunia, kitovu cha mgogoro wa miaka mingi kati ya makabila ya Lendu na Hema katika jimbo tajiri la mafuta la Ituri kuwezesha waathirika kufuatilia kwa urahisi mwenendo wa kesi hiyo.

NTAGANDA anakabiliwa na mashtaka 18 ya uhalifu wa kivita na dhidi ya binadamu kwa mchango wake katika mgogoro huo lakini mwenyewe amekanusha madai hayo.

Mahakama hiyo ambayo kwa sehemu kubwa imeshutumiwa barani Afrika kwa kuwa taasisi inayotawaliwa na ukoloni mamboleo wa nchi za Ulaya mara nyingi imetakiwa kusogeza kazi zake karibu na waathirika wa vitendo vya uhalifu wa kivita na binadamu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment