Image
Image

Asilimia 73 ya maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI yanayowakumba baadhi ya vijana Barani Afrika huwapata wasichana.


Asilimia 73 ya maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI  yanayowakumba  baadhi ya vijana Barani Afrika huwapata wasichana  huku asilimia 15 ya vijana wote  ndiyo wanaotambua hadhi yao na hivyo kusababisha  tatizo hilo kuendelea kuwa kubwa.
Hayo yamesemwa  na Mke wa Rais,Mama SALMA KIKWETE alipokuwa akizungumza  kwenye mkutano wa 15 wa Umoja wa wake wa Marais wa Afrika wa Kupambana na UKIMWI uliofanyika Sandton, Jijini Johannesburg,  Afrika Kusini.
Mama KIKWETE ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo  amesema tatizo la Virusi vya UKIMWI na UKIMWI bado ni kubwa miongoni mwa vijana wa kike na kama wataendelea kuambukizwa kwa kiwango hicho kutakuwa na muda mrefu wa kupambana na maambukizi kwa wenzao.
Akiwakaribisha wake hao wa Marais, Mke wa Rais wa Afrika  Kusini Mama THOBEKA MADIBA ZUMA amesema muda umefika kwa wao  kuonesha majukumu yao  katika Bara la Afrika kwa kuungana na viongozi wa jamii zao ili kuondoa unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake zikiwemo mila kandamizi, kusimamia ili wanawake wapate haki za uchumi, afya ya uzazi na kulinda haki za  wazee, walemavu na watoto.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment