Image
Image

Wizara ya maliasili yakiri upungufu mkubwa wa kifuta machozi kwa mtu aliyejeruhiwa au kuuawa na mnyamapori.


Wizara ya Maliasili na Utalii imekiri kuwa  kanuni za malipo ya kifuta machozi iliyoanza kutumika  Aprili 2011 kuwa na  upungufu mkubwa,  ikiwemo viwango vidogo vya kufuta machozi kwa mtu aliyejeruhiwa au kuuawa na mnyamapori.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,  MAHAMOUD MGIMWA amesema hayo alipokuwa  akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum,  PAULINE GEKUL aliyetaka kujua ni lini kanuni za maliasili za mwaka 2011 zinazotumika kulipa fidia kwa wananchi pale ambapo mazao yao yataharibiwa na wanyapori zitarekebishwa kutokana na upungufu uliyojitokeza.
Amesema zoezi la kurejea kanuni linaendelea kutokana na mchakto wake kuhusisha hatua mbalimbali ikiwemo ushirikishwaji wa wadau  mbalimbali.
Bunge limeelezwa kuwa vikundi vya vijana 31 vimenufaika na huduma mbalimbali ikiwemo mikopo ya  Shilingi Milioni 16.402,vifaa na mafunzo mbalimbali ya ujasiriamali.
Naibu Waziri wa Fedha  na Uchumi, ADAM MALIMA ametoa kauli hiyo alipokuwa  akijibu swali la mbunge wa Viti maalum,  LETICI NYERERE aliyeuliza Serikali imetoa huduma gani kwa vijana wa wilaya ya Kwimba ili kuwezesha kujiajiri wenyewe na vikundi gani vimenufaika na mpango huo.
Amesema kutoa huduma ya mikopo yenye masharti nafuu kupitia mfuko wa maendeleo ya vijana pamoja na kuta nyenzo za kufanyia kazi ambapo vikundi vya vijana kutoka vijiji vitatu vilipatiwa mashine nne za kufyatua matofali kutoka Shirika la Nyumba la Taifa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment