Image
Image

Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo kuanza miradi ya utunzaji na uhifadhi wa matunda na mboga.


Wizara ya Viwanda  na Biashara kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo,Chakula na Ushirika pamoja na Chama cha Wakulima wa mboga, imeanzisha miradi kadhaa ya chakula kwa ajili ya utunzaji na uhifadhi  wa matunda na mboga katika maeneo mbalimbali nchni ili kupunguza uharibifu.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje,MAHADH JUMA MAALIM, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara ametoa kauli hiyo alipokuwa  akijibu swali la Mbunge wa Mkanyagaeni,MOHAMED MNYAA aliyeuliza kwa nini Wizara ya Viwanda na Biashara isitoe elimu kwa wakulima namna ya kuhifadhi matunda  hapa nchni kufikia muda angalau wa miezi mine bila ya kuharibika.

Amesema Serikali imekamilisha jengo la kuhifadhi mboga na matunda na kuweka kontena la baridi kwa gharama ya Shilingi  zaidi ya Milioni 400 litakalohudumia vikundi 85 vya wakulima wa wilaya ya Lushoto na Korogwe.

Bunge  limeelezwa Shirika la Umeme Nchni -TANESCO- limekamilisha kuandaa hadidu za rejea kwa ajili ya kutangaza zabuni ili kumpata mshauri mwelekezi atakayefanya upembuzi yakinifu wa ujenzi wa mitambo ya kufua umeme wa makaa ya Mawe ya Ngaka itakayojengwa katika kijiji cha Ntunduwaro Wilayani Mbinga.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment