Image
Image

Serikali Mkoani Kigoma,kuwakamata waomba hifadhi kutoka Burundi,ambao wametoroka na kuishi nchini kinyume cha Sheria.


Serikali Mkoani Kigoma, imeahidi kuwakamata waomba hifadhi kutoka Burundi, ambao wametoroka na kuishi nchini kinyume cha sheria hali iliyosababisha kuenea ugonjwa wa Kipindupindu mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteini-Kanali mstaafu ISSA MACHIBYA amesema waomba hifadhi wengi ambao idadi yao haijajulikana hawajasajiliwa na kwamba waliondoka katika maeneo ya mapokezi hasa katika kijiji cha kagunga na kuchanganyikia na wananchi katika maeneo mbalimbali ya vijiji hali iliyochangia kuenea kwa ugonjwa wa Kipindupindu.
Mkuu huyo wa Mkoa wa Kigoma ameeleza hayo katika kikao cha kamati ya afya ya mkoa  amesema serikali itahakikisha wakimbizi hao takriban Elfu-30  ambao wametorokea katika maeneo mbalimbali nchini wanatafutwa na kuchukuliwa hatua za sheria.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Dakta  LENARD SUBI ameeleza kuwa wananchi katika vijiji vilivyokumbwa na ugonjwa wa Kipindupindu kwa msaada wa Shirika la Afya Duniani  watapatiwa chanjo ili kuzuia ugonjwa huo kuenea zaidi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment