Image
Image

Rais Kikwete awaapisha Majaji wapya wawili wa mahakama ya rufaa ikulu jijini Dar Es Salaam.


Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha Mhe. Stella Mugasha- Jaji Mteule wa Mahakama ya Rufani, Ikulu jijini Dar es salaam Juni 16, 2015. Kabla ya uteuzi wake Mhe. Jaji Mugasha alikuwa Jaji Mfawidhi Mahakama kuu- Kanda ya Dar es Salaam.
Mhe. Jaji Mugasha akitia sahihi hati ya kiapo mara baada ya kuapishwa rasmi na Mhe. Rais Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam.
Dar es Salaam.
Majaji wapya wawili wa mahakama ya rufaa Augustine Mwarija na Stella-Esther  Mugasha wamesema changamoto inayowakabili ni ya kuhakikisha haki inatendeka na kwa wakati ikiwa ni pamoja na kuondoa msongamano wa mashauri.

Majaji hao wameyasema hayo ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kuapishwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa majaji wa mahakama ya rufaa wakitokea mahakama kuu ambapo Mwarija, alikuwa jaji mfawidhi, mahakama kuu, divisheni ya biashara huku mugasha akiwa  jaji mfawidhi mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam.

Wakizungumza katika hafla fupi iliyofanyika ikulu majaji hao wameahidi kutumia uzoefu walionao katika kukabiliana na changamoto ya wingi wa mashauri katika mahakama hiyo kwa kutumia utaratibu wa kushughulikia kwanza mashauri ya yaliyochukuwa muda mrefu kutolewa maamuzi.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment