Amesema anayo kura moja tu ambayo
ataitumia mwezi ujao wakati wa vikao mbalimbali kuamua nani awe mgombea Urais
wa Chama cha Mapinduzi katika Uchaguzi
Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu
kwa vyombo vya Habari, Rais KIKWETE ameyasema hayo Mjini Johannesburg, Afrika
Kusini alipokuwa akizungumza na Waziri
Mdogo wa Mambo ya Nje wa Marekani, anayeongoza Kitengo cha Masuala ya Afrika
Bi. LINDA THOMAS-GREENFIELD.
Pia amesema hana tatizo na
kujitokeza kwa wagombea wengi wa nafasi ya Urais zamu hii kupitia Chama cha
Mapinduzi kwa sababu huwezi kuwazuia
watu kugombea nafasi hiyo kwa sababu ni haki yao.
Viongozi hao wawili walikuwa
wanahudhuria Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika
kwenye Kituo cha Mikutano cha Sandton Mjini Johannesburg, Afrika Kusini.
0 comments:
Post a Comment