Image
Image

Serikali kuboresha miumbombinu ya Tehama na kuwajengea wanafunzi uwezo wa kusoma na kupata taarifa hapa nchini.


Serikali imesema itaendelea kuboresha miumbombinu ya Tehama katika shule mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na kuwajengea wanafunzi uwezo wa kusoma na kupata taarifa mbalimbali zitakazo wasaidia katika masomo yao kwa nyia ya Tehama.
Kauli hiyo ya serikali imetolewa jijini Dar es Salaam na katibu mkuu wa wizara ya mawasiliano,sayansi na tekinolojia Proffesa .Patrick Makungu muda mfupi baada ya kuzindua mpango wa matumizi ya Compyuta katika shule za wanafunzi wenye mahitaji maalum na mchanganyiko ambapo amesisitiza ni lengo la serikali kuona kila mwanafunzi ananufaika na mfumo wa Tehama.
Kwa upande wake afisa mtendaji mkuu wa mfuko wa mawasiliano kwa umma Enginea Peter ulanga amesema ni lengo la taasisi yake kuhakikisha inafikia shule zaidi ya shule 200 za wanafunzi wenye mahitaji maalum ili kuwawezesha waendane na changamoto za ukuwaji wa tekinolojia.
Jumla ya shule 4 za watoto wenye mahitaji maalum zimenufaika na mradi huo ambapo kompyuta zaidi ya 35 zimetolewa kwa shule hizo huku mwalimu mkuu wa shule ya uhuru mchangayiko akielezea jinsi walivyo nufaika na mradi huo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment