Image
Image

Sheria kuwanyima haki ya kupiga kura wafungwa.


Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) imesema wafungwa hawatapiga kura katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 25 kwa sababu sheria inayoweza kuwapa fursa hiyo haijafanyiwa marekebisho.
Hayo yalisemwa jana na mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa.
“Sheria haijabadilishwa ili kuruhusu vituo vya kupigia kura katika magereza na monitoring (uangalizi).  
Pia kunatakiwa kuwe na vibali kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani,” alisema Jaji Lubuva.
Alisema bado hawajakutana na Serikali kujadili suala hilo.
“Tukishakaa pamoja sasa tutakuwa na cha kuwaambia wananchi,” alisema.
Hivi karibuni Kamati Kuu ya CCM iliishauri serikali kukaa na Nec na kutafuta njia muafaka ya kulishughulikia kwa kuzingatia maslahi mapana ya Taifa.
Akizungumzia changamoto, Jaji Lubuva alisema suala la watu kuchukua muda mrefu katika uandikishaji hutokea wakati mashine zinapokuwa na tatizo.
“Mtu mmoja anachukua dakika mbili hadi nne kuandikishwa, labda panapotokea tatizo katika mashine ama uchukuaji wa alama za vidole lakini maofisa waandikishaji hulitatua kwa kipindi kifupi,” alisema.
Kuhusu baadhi ya watu kuachwa bila kuandikishwa, Jaji Lubuva alisema hakuna mtu aliyeachwa kituoni bila kuandikishwa.
“Kilichojitokeza baadhi ya viongozi wa kisiasa huenda kwa wananchi na kuwauliza nani aliyeachwa bila kuandikishwa, lakini si kwamba waliokwenda vituoni hawakuandishwa,” alisema.
Jaji Lubuva alisema malalamiko yaliyotolewa na katibu mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa kuhusu haki ya wanafunzi wa vyuo vikuu kuandikishwa, siyo ya kweli.
Alisema wanafunzi hao pamoja na wananchi wengine wanayo nafasi ya kubadilisha taarifa zao muda wowote.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment