Image
Image

Silima:Vitambulisho vya Taifa vingetumika kupiga kura.


Naibu Waziri wa Mambo ya ndani ya  Nchi, Pereira Ame Silima, (pichani), amesema moja ya mambo ambayo hayakufanyika vizuri mwanzoni wakati wa uandikishaji wa vitambulisho vya Taifa ni kutovifanya vitumike kupiga kura katika uchaguzi mkuu.
Amesema kama kitambulisho hicho kingeboreshwa kingeweza kutumika kwa ajili ya kupiga kura, hivyo kusingekuwapo uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura.
Waziri huyo aliyasema hayo jijini Dar es Salaam, wakati wa ufunguzi wa kongamano la kimataifa la uandikishaji wa vitambulisho vya Taifa lijulikanalo kama ‘Govetnment Forum on Electronic Identity in Africa', unaofanyika Afrika kwa mara ya kwanza na kujumuisha wataalam zaidi ya 300 wa ndani na nje ya Afrika.
“Kama tungejipanga mwanzo vizuri ni wazi kusingekuwapo haja ya mchakato unaoendelea wa kuandikisha kwa kutumia BVR, ni nafasi kwetu kujifunza na kujirekebisha na pia watajifunza kutoka Tanzania,” alisema.
Silima alisema siku zijazo vitambulisho hivyo vitaboresha zaidi ili kutumika kwenye maeneo mbalimbali, na kwamba kwa siku za usoni vitatumika kwenye malipo mbalimbali.
Aliwataka Watanzania wanaoshiriki katika kongamano hilo kupokea na kutumia teknolojia inayotoka kwenye makampuni mbalimbali duniani.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), Dickson Maimu, alisema watu milioni 6.1 wameandikishwa katika maeneo ya Zanzibar, Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara, Morogoro na Tanga na kwamba watu milioni 2.5 wamepatiwa vitambulisho.
Alisema kongamano hilo linalojulikana ‘Govetnment Forum on Electronic Identity in Africa’, limeleta pamoja nchi 24 ambazo zitajadili kwa kina changamoto zilizopo kwenye uandikishaji, uandaaji wa vitambulisho vya Taifa na jinsi gani vitatumika kwa maendeleo ya Taifa.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment