Wizara ya Elimu ya
nchi hiyo, imetoa muda wa miaka mitatu kwa shule za msingi za bweni kufunga
huduma hiyo.
Lengo la Serikali ya Rwanda ni kutaka kuona
watoto wakipata muda zaidi wa kukaa na wazazi wao, kuwafinyanga kimalezi mpaka
wafikie umri wa kujitambua zaidi.
Hivyo kwa serikali ya Rwanda muda mwafaka wa
wanafunzi kwenda shule za bweni ni pale wanapofika sekondari.
Upepo wa shule za bweni kwa wanafunzi wenye
umri mdogo umeikumba pia Tanzania. Hivi sasa kuna idadi kubwa ya shule
zinazopokea wanafunzi chini ya miaka 10 wanaosoma elimu ya msingi. Je, ni
mwafaka kwa Serikali ya Tanzania kufuata nyayo za Rwanda kuzuia shule hizo?
Utengano na wazazi
Hapa nchini, wanafunzi wanatumia miezi si
chini ya tisa wakiwa shuleni, muda ambao Meneja wa utafiti na
uchambuzi wa sera wa shirika la HakiElimu, Godfrey Boniventure anasema hauwapi
watoto nafasi ya malezi kutoka kwa wazazi
“Miezi tisa ni mingi kwa mtoto kuwa
mbali na malezi ya wazazi, kwa hivyo nakubaliana na mabadiliko ya Rwanda;
ingetokea hapa nchini ingesaidia japokuwa ninaamini haiwezekani
kutokana na changamoto ya umbali wa shule nyingi zilivyojengwa
ambazo zinalazimisha kuwa na bweni japo si vizuri kimalezi,’’ anasema na
kuongeza:
“Kiuzoefu, watoto wengi wanaosoma shule
za bweni huathirika kimalezi; wanabadilika tabia bila mzazi kujua lakini kama
mwanafunzi anakwenda shule na kurudi, ni rahisi kwa mzazi kutambua
mabadiliko na mwenendo wake.”
Anasema hata Korea Kusini ni miongoni mwa
mataifa yaliyoendelea, lakini hayatumii mfumo wa shule za bweni ila kwa
wanafunzi maalumu, kama anavyofafanua:
“Korea Kusini wanatumia shule za bweni kulea
vipaji na si kwa masomo ya sekondari au shule ya msingi, vipaji ndiyo vinalelewa,
kukuzwa ili kulinda visipotee.’’
Katibu Mkuu wa Umoja wa wamiliki wa shule na
vyuo binafsi nchini (Tamongsco), Benjamin Nkonya, anasema uamuzi wa kufungia
shule za bweni kwa daraja la elimu ya msingi ni sahihi.
“Kuanzia kidato cha kwanza mpaka vyuoni
inawezekana kukaa bweni na kwa Tanzania tunaweza kufanya hivyo, lakini lazima
kuwapo na huduma nzuri za usafiri wa mabasi ya wanafunzi kwa wanafunzi wa shule
za kwenda na kurudi nyumbani,’’anasema.
0 comments:
Post a Comment