Stars ambayo iliingia kambini
jijini Dar es Salaam kwa awamu mbili imegawanywa katika makundi mawili ambapo
kundi la kwanza lenye wachezaji 23 linaloundwa na wachezaji wanaocheza ndani na
nje ya nchi litaondoka Alhamisi kwenda kujichimbia nchini Ethiopia kujiwinda
dhidi ya timu ya mafarao wa misri katika mchezo wa kuwania tiketi ya kushiriki
fainali za Afrika-Afcon utakaochezwa jijini Alexadria, Misri.
Wakati kundi la kwanza litaongozwa na kocha mkuu
mholanzi Mart Nooij atakayesaidiwa na Mecky Mexime, kundi la pili
litakaloondoka nchini ijumaa litakuwa chini ya kocha Salum mayanga na baada ya
kurejea nchini baadhi ya wachezaji watajumuishwa na wenzao waliokuwa misri kwa
ajili ya mchezo wa kusaka tiketi ya kucheza fainali za Afrika kwa wachezaji wa
ndani-chan dhidi ya uganda THE CRANES utakaochezwa juni 20 kwenye uwanja wa
amaan kisiwani Zanzibar..
0 comments:
Post a Comment