Image
Image

Michuano ya mpira wa kikapu maarufu kama BBALL kitaa kuzinduliwa ijumaa.


Michuano ya mpira wa kikapu maarufu kama BBALL kitaa ngazi ya kanda inatarajiwa kuzinduliwa ijumaa  ambapo kutakuwa na pambano kali litakalo zikutanisha timu kutoka kanda ya mashariki ambayo inaundwa na wachezaji kutoka msasani, Oysterbay na Masaki dhidiya timu kutoka kanda ya pili ya magharibi ambayo inaundwa na wachezaji kutoka mbezi beach, kunduchi na tegeta.
Mratibu wa wa bball kitaa karaban ikarabani  amesema pambano hilo ambalo linatarajiwa kuvuta hisia za maelfu ya mashabiki kutoka wilaya zote za jiji la Dar es salaam yaani kinondoni, temeke na ilala litafanyika katika uwanja wa bball kitaa Park, uliopo  karibu na ukumbi maarufu wa Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Karabani pia alizitaja kanda zingine ambazo zitashiriki katika michuano hiyo mwezi julai kuwa, ni mabingwa watetezi kanda ya nne ya mashariki inayoundwa na wachezaji kutoka temeke na mbagala  kanda ya kwanza ya
Mashariki, kanda ya tatu ya mashariki, kanda ya pili ya magharibi, kanda ya tatu ya magharibi na kanda ya kanda ya nne ya magharibi. Mshindi wa michuano hii ya nnen gazi ya kanda atakabidhiwa kitita cha shilingi milioni 5.
Kwa upande wake, meneja bidhaa wa coca-cola nchini maurice njowoka amsema kuwa kampuni ya coca-cola kupitai kinywaji cha sprite imejiona ni yenye heshima kubwa mara baada ya kupewa fursa ya kudhamini michuano hiyo nchini na kuahidi kuwa kampuni yake kuendelea kutoa ushirikiano wa bega kwa bega kuhakikisha kuwa mchezo huu unazidi kusonga mbele.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment