Image
Image

MAREKANI:Hatupo tayari kuona Nkurunziza anaongezewa madaraka.


Marekani imesema mpango wa Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi kugombea Muhula wa tatu, unahujumu hali ya utulivu nchini humo na ni kinyume na mkataba wa amani wa Arusha uliomaliza vita vya miaka 13 vya wenyewe kwa wenyewe katika taifa hilo.
Taarifa iliyotolewa na ubalozi wa marekani mjini Bujumbura, imemtaka Rais Nkurunziza azingatie upya azma  yake hiyo ili kuunusuru mkataba wa Arusha.
Vyama vya upinzani na jumuiya za kiraia nchini humo vinasema mpango wa kiongozi huyo unakiuka katiba inayosisitiza juu ya mihula miwili na pia makubaliano ya amani ya Arusha.
Rais Nkurunziza anadai muhula wa kwanza alichaguliwa na bunge na sio umma.
Uchaguzi wa bunge nchini Burundi unatarajiwa kufanyika tarehe 5 mwezi huu ukifuatiwa na  wa rais juni 26.
Taarifa ya  marekani imetolewa baaada ya mkutano wa kilele wa viongozi wa kanda hiyo kuhusu Burundi, uliofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa juma kutaka uchaguzi uahirishwe hadi katikati ya mwezi julai.
Marekani pia imejiunga na wale wanaotoa wito kutoka uchaguzi uahirishwe.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment