Image
Image

Uandikishaji BVR Dar majanga.


Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) itatakiwa kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha inatimiza mipango yake kuelekea katika Uchaguzi Mkuu kutokana na ugumu unaoweza kutokea katika kukamilisha uandikishaji wapigakura katika jiji la Dar es Salaam na ugawaji wa mipaka ya majimbo nchini.
Ratiba ya uandikishaji ya NEC imelipatia jiji la Dar es Salaam siku 13 za kuandikishaji wapigakura kwa kutumia teknolojia ya Biometric Voters Registration (BVR).
Siku hizo ni pungufu kwa wastani wa siku 16 zilizotumika kwenye mikoa mingine nchini ambayo mingi ina nusu ya idadi ya watu wenye umri wa kupiga kura ikilinganishwa na jiji la Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Chama cha NCCR-Mageuzi Mosena Nyambabe aliliambia gazeti hili kuwa ili NEC iendane na kasi ya muda uliopo, inatakiwa kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha inakamilisha uandikishaji wapigakura na ugawaji wa mipaka ya majimbo.
“Uzuri wa Dar es Salaam ni makao makuu ya kila kitu, tutaangalia mwenendo wa uandikishaji kujua unafanyika kikamilifu au la na utatupa picha hali ilikuwaje katika mikoa mingine. Bado wana kazi kubwa kwa sababu hawajakamilisha kuchora ramani ya mikoa na majimbo…lazima wafanye kazi ya kutisha,” alisema Nyambabe.
Alisema kazi ya mwaka mmoja na nusu haiwezi kufanyika ndani ya wiki mbili ndiyo maana wakati mwingine huwa wanaona mipango ya NEC kama viini macho. Hata hivyo akasema angalau sasa NEC wamejikita katika Uchaguzi Mkuu kuliko Kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa.
Takwimu zinasemaje?
Takwimu za Shirika la Takwimu la Taifa (NBS) za makadirio ya watu wenye sifa ya kupiga kura zinaonyesha kuwa Dar es Salaam ina zaidi ya watu 2.93 milioni, idadi ambayo ni sawa na jumla ya wapigakura katika mikoa sita ya Katavi, Lindi, Shinyanga, Njombe, Iringa na Rukwa ambao wanakadiriwa kuwa 2.94 milioni.
NBS inakadiria Morogoro kuwa na wapigakura zaidi ya 1.28 milioni wakati Tanga ina watu zaidi ya 1.12 milioni.
NEC kupitia ratiba hiyo iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura, Ruth Masham, ilionyesha mikoa mingi nchini imepatiwa siku kati ya 28 na 30 kuandikisha wapigakura wakati katika mikoa hiyo kukiwa hakuna mkoa unaozidi makadirio ya watu 1.5 milioni.
Dar es Salaam itaanza shughuli ya uandikisha Julai 4 hadi Julai 16 mwaka huu wakati huo huo mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Mara na Manyara iliyoanza Juni 12 nayo itakuwa ikiendelea kuandikisha hadi Julai, 12.
NEC ambayo ilishapokea mashine zote za BVR 8,000, itakuwa ikiendelea kuandikisha mikoa ya Morogoro, Pwani na Tanga itakayoanza Juni 18 hadi Julai, 18 siku mbili baada ya Dar es Salaam kumaliza uandikishaji kwa mujibu wa ratiba hiyo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment