Image
Image

Profesa Tibaijuka azomewa kwao mbele ya Kinana.


Mbunge wa Muleba Kusini (CCM), Profesa Anna Tibaijuka jana alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuzomewa na wananchi wa jimbo lake mbele ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
Hali hiyo ilijitokeza jana asubuhi katika Kata ya Nshamba wilayani hapa wakati msafara wa Kinana ulipofika kuzindua mradi wa maji. Kadhia hiyo ilianza baada ya Katibu wa CCM Mkoa wa Kagera, Ally Idd Ame kumkaribisha mbunge huyo ili awasalimie wananchi. Hata hivyo, wananchi hao walianza kuzomea kwa zaidi ya sekunde 40 wakipinga Profesa Tibaijuka kupanda jukwaani, hali iliyomlazimu Mkuu wa Wilaya, Francis Isack kupanda jukwaani na kutoa kauli ya kiutawala ili kuwanyamazisha wananchi hao.
“Anayetaka kusikiliza abaki na asiyetaka aondoke,” alisema Isack na kuwanyamazisha mamia ya wananchi hao. Baada ya kauli hiyo wananchi walitulia na kuruhusu Profesa Tibaijuka kupanda na kuhutubia kwa muda.
“Kama hamnitaki siyo lazima niwe mbunge wenu, mnaruhusiwa kubadili. Huyo aliyewapa viroba asubuhi hii ili mje mnitie aibu mbele ya katibu mkuu wa chama nawaambia hiyo dhambi itawatafuna,” alisema.
Aliwaambia wananchi hao kuwa anachokifanya ni kuwatumikia na kuwaletea maendeleo, hasa wanawake...
“Mimi sitafuti kazi na wala sina njaa... na kama hela ya kula ninayo. Mimi sigangi njaa na kama mnataka kuwa na kiongozi mganga njaa muwekeni muone atawasaidia vipi,” alisema.
Akihitimisha salamu zake kwa wananchi hao alisema kama wana jambo lao la ziada walifanye lakini wamuache aendelee na jitihada za kuwaletea wanawake maji... “Sina kinyongo na yeyote kwa sababu “I am too sophisticated (mstaarabu). Nipo juu ya mambo madogomadogo yanayowasumbua.”
Mbunge huyo ambaye hivi karibuni aliondolewa uwaziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kutokana na kashfa ya Tegeta Escrow, alimweleza Kinana kuwa eneo hilo limekumbwa na upinzani kutoka kwa mtu anayehitaji kulichukua ambaye ni kutoka ndani ya CCM.
Profesa Tibaijuka alisema katika ubunge wake amefufua mradi huo wa maji utakaogharimu Sh200 milioni kupitia shirika moja ambalo mkandarasi wake ni wa Umoja wa Mataifa na utekelezaji umeanza miezi minne iliyopita lakini unahujumiwa.
“Mradi huu wa Nshamba unahujumiwa na wapinzani wangu kutoka ndani ya CCM na vyama rafiki vya kisiasa, lakini lengo lao ni kunidhoofisha kisiasa, jambo ambalo linadidimiza maendeleo,” alisema Profesa Tibaijuka ambaye aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Makazi la Umoja wa Mataifa (UN – Habitat).
Kinana na kahawa
Katika ziara hiyo, Kinana aliitaka Serikali mkoani Kagera kusimamia wakulima kuuza kahawa ndani na nje ya nchi ili wanufaike badala ya kuwahusisha na magendo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment