Image
Image

Wananchi wa Mtwara watoa ardhi Ekari 2500 kwa ujenzi wa bandari*Wakanusha kauli ya Mdee kuwa wanarubuniwa kuuza ardhi.


Wananchi wa vijiji vya Mgao na Kisiwa ,katika  Kata ya Naumbu Mtwara Vijijini wamesema kwa hiari yao wameridhia kutoa  ardhi  Ekari Elfu- mbili na 500 kwa ajili ya ujenzi wa bandari  na tayari taratibu za kupata stahiki  zao zinaendelea .
Wananchi hao wamekanusha  kauli ya Mbunge wa Kawe ,HALIMA MDEE aliyedai wamerubuniwa na kuuza ardhi hiyo kwa bei poa.
Kauli hiyo ya wananchi imekuja baada ya mbunge huyo  kutoa kauli za kulalamikia uuzwaji holela wa ardhi ,ikiwemo ya vijiji hivyo bungeni wakati akichangia hoja katika Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Wakizungumza kwa masikitiko baadhi ya wananchi na viongozi wao wamelaani kauli za baadhi ya wanasiasa  ambazo wakati mwingine  wamesema  zina weza kuzua  migogoro.
Akizungumzia hilo Meneja wa Bandari Mkoa wa Mtwara ,ABELI MWASENGA amesema upimaji wa eneo waliotoa kwa ajili ya ujenzi wa bandari unaendelea vizuri na mara utakapokamilika wanatarajia kutoa fidia kwa wakazi wa vijiji vya Mgao na Kisiwa.
Kijiji cha mgano kimetoa ekari  1,500  wakati kijiji cha Kisiwa kimetoa Ekari Elfu moja kwa ajili ya ujenzi wa bandari itakayomilikiwa na  mwekezaji wa kiwancha cha saruji   Al - Haji ALIKO DANGOTE.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment