Wasichana hao wenye umri wa
kati ya miaka 22 hadi 30 hivi sasa ni kutoka Chad, Sierra Leone, Somalia na
Uganda wanatuma ujumbe huo kupitia akaunti hiyo yenye wafuasi zaidi ya Milioni
Nne ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya mtoto wa Afrika.
Miongoni ni Jennifer kutoka
Uganda ambaye anasema alitekwa akiwa na umri wa miaka 13 na kuozwa kinguvu
akiwa na umri wa miaka 14 huko Sudan kwa kamanda wa waasi wa Lord's Resistance
Army.
Amesema simulizi yake ni
fursa pekee kuchangia kampeni ya kutokomeza ndoa za utotoni barani Afrika.
Takwimu zinaonyesha kuwa
duniani kote zaidi ya wanawake Milioni 700 walioko hai hivi sasa waliozwa
utotoni na wengi wao wako nchi za Afrika kusini mwa jangwa la Sahara.
0 comments:
Post a Comment