Watu kumi wamefariki
dunia papo hapo na wengine 47 kujeruhiwa baada ya basi la kampuni ya Simiyu Express
lililokuwa likitokea bariadi mkoani Simiyu kuelekea jijini Dar es Salaam
kupasuka gurudumu la mbele ka kupoteza muelekeo na kisha kuparamia mti katika
kijiji cha wilunze eneo la Chalinze nyama wilayani Chamwino Dodoma.
Kwa mujibu wa mashuhuda wamesema kabla ya ajali basi hilo lenye namba za usajili T318 ABM SCANIA lilikuwa kwenye mwendo mkali na wakasikia kishindo cha kupasuka Gurudumu na kupoteza muelekeo umbali wa zaidi ya mita 800 kisha kugonga mti wa mbuyu ambapo watu kumi walifariki dunia papo hapo huku idadi kubwa ya majeruhi ikiokolewa.
Kwa mujibu wa mashuhuda wamesema kabla ya ajali basi hilo lenye namba za usajili T318 ABM SCANIA lilikuwa kwenye mwendo mkali na wakasikia kishindo cha kupasuka Gurudumu na kupoteza muelekeo umbali wa zaidi ya mita 800 kisha kugonga mti wa mbuyu ambapo watu kumi walifariki dunia papo hapo huku idadi kubwa ya majeruhi ikiokolewa.
Akizungumzia chanzo cha
ajali hiyo kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma kamishina msaidizi David Mnyambugha
amesema ni mwendo kasi ambapo mara baada ya gurudumu kupasuka dereva
alishindwa kulimiliki na ndipo likapoteza mwelekeo.
Kwa upande wake mganga
mkuu wa mkoa wa dodoma Dk.Ezekiel Mpuya amethibitisha kupokea majeruhi 47 na
miili 10 ya waliofariki dunia akiwemo dereva wa basi hilo aliyetambulika kwa
jina la Salum Ramadhani shafi huku majeruhi waliolazwa kwenye hosipitali ya
rufaa ya mkoa wa dodoma wakieleza namna ajali hiyo ilivyotokea.
Kwa
upande wake mkuu wa mkoa wa Dodoma Chiku Galawa ambaye pia ni mwenyekiti wa
kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa akizungumza katika eneo la ajali wamewataka
wasafiri kutoa taarifa za mienendo mibovu ya madereva wawapo barabarani huku
akitoa wito kwa wakazi wa dodoma na wasamaria wema kujitokeza kutoa misaada ya
hali na mali kwa majeruhi pamoja na kutambua miili ya marehemu.
0 comments:
Post a Comment