Image
Image

Serena Williams na Maria Sharapova watinga mzunguko wa tatu wa michuano ya Wimbledon.


Mchezaji namba moja wa tennis kwa wanawake serena williams na mchezaji namba nne maria sharapova wametinga hatua ya mzunguko wa tatu wa michuano ya wimbledon kwa ushindi wa seti mfululizo.

Willaims alimchapa timea babos seti 6-3 6-1 huku kukiwa na joto kali na sasa anakutana na irina-camelia begu.

Wakati huo huo dada yaje serena, venus williams na viktoria azarenka pia walifanikiwa kusonga mbele lakini mchezaji namba saba kwa ubora ana ivanovic akatolewa kwenye michuano hiyo.

Kwingineko meneja wa timu ya soka ya wanawake ya uingereza Mark Sampson amesema uingereza wanapaswa kupokelewa nyumbani kama mashujaa pamoja na kutolewa kwenye michuano ya kombe la dunia la wanawake baada ya kupokwa kichapo cha goli 2 kwa 1 kutoka kwa japan.


Uingereza walijitahidi kuwazuia mabingaw watetezi wa kombe hilo japan mpaka dakika ya 90 kabla ya beko laura bassett kujifunga kwenye dakika za nyongeza.

Simpsom alisema inahuzunisha sana lakini bado timu hiyo imeonesha uimara na ushujaa mkubwa kwani imeweka historia ya kutinga nusu fainali za michuano hiyo kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwake.

Na katika dondoo za usajili bayern munich ya nchini ujerumani imemsajili kiungo wa Shkhtar Doneitsk Mbrazil Douglas costa kwa dau la paundi milioni 21.

Kusajiliwa kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 kunaongeza uwezekano wa kiungo bastian shwensteiger kuhamia Manchester United.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment