KAIMU Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF),
Jemedari Said amelalamikia kitendo cha viongozi wa klabu za Ligi Kuu
kutokuwa na ushirikiano katika masuala muhimu.
Akizungumza ofisini kwake jana, Said alisema viongozi
wengi wa klabu za Ligi Kuu wamekuwa wa kwanza kulalamika na kuitupia
lawama TFF wakati wao wenyewe si watu wa kutilia maanani kwenye masuala
muhimu.
“Imekuwa kawaida kwa viongozi wa klabu likitokea jambo ni wa kwanza
kulaumu TFF wakati wao kuna masuala muhimu ni wagumu kuyatekeleza hata
kama yanahitaji jambo kidogo sana,” alisema.
Akifafanua kauli hiyo, Said alisema imepita zaidi ya wiki viongozi wa
klabu waliombwa majina ya makocha wao wa makipa kwa ajili ya kozi ya
Fifa lakini mpaka kufikia jana ni klabu mbili pekee za JKT Ruvu na
Majimaji ndizo zilizoitikia mwito.
“Unaona hii kozi ni makocha wa makipa itaendeshwa na Fifa mwishoni
mwa mwezi huu, taarifa viongozi wote wanazo lakini kuinua simu tu au
kunitumia ujumbe kwamba timu fulani kocha wetu ni fulani hawawezi
kufanya hivyo… “Hivi hapa ndio nina kazi ya kuwapigia simu mmoja mmoja
kuwauliza kuhusu jina la kocha wao wa makipa, kitu muhimu kama hiki
lakini hawakitilii maanani… “Kwa mfano kama Yanga tunajua kwamba kocha
wao wa makipa ni Pondamali (Juma) taarifa walikuwa nayo kama zilivyo
klabu nyingine, lakini leo (jana) mapema asubuhi niliwapigia simu wanipe
jina la kocha wao lakini mpaka saa nane hii mchana nazungumza na wewe
hawajanipa, ugumu uko wapi,” alisema.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment