Image
Image

JK kuzindua benki ya kilimo.

RAIS Jakaya Kikwete anatarajiwa kuzindua rasmi benki ya kwanza ya Maendeleo ya Kilimo nchini kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam kesho.
Akizungumza jana, Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo, Thomas Samkyi, alisema dhumuni kuu la uanzishaji wa benki hiyo ni kuboresha tija katika uzalishaji kwenye sekta ya kilimo kwa kuunganisha nguvu za wadau mbalimbal.
Alisema benki hiyo itaendeleza miundombinu ya kilimo kama miradi ya umwagiaji, usafirishaji, uhifadhi na mindombinu ya masoko, ambayo inachangia maendeleo ya sekta ya kilimo. Aliongeza kuwa benki hiyo inalenga kuziba mianya mikubwa ya ukopeshaji kwenye kilimo, ambayo inaachwa na benki za biashara.
Aidha, alisema benki hiyo itachochea kukua kwa sekta ya kilimo kwa kutoa mikopo wakulima, ambao wengi wao hawana uwezo wa kupata huduma za kibenki. “Benki hii imeundwa ili kutoa mikopo kwa masharti nafuu na kutoa huduma nyinginezo zitakazoongeza uwezo wa wakulima kukopa na kuzalisha na ili kufanikisha hilo benki inabidi iwe na vyanzo endelevu vya fedha za kutosha kwani nchi hii ni kubwa na wadau wa benki ni wengi,” aliongeza Samkyi.
Aliongeza kuwa itakuwa ikifanya kazi kwa ukaribu zaidi na benki washirika, ambao watafanya nao kazi katika kuwakopesha wakulima hao. Alisema watafungua ofisi kwa kanda na kutakuwa na utaratibu maalumu wa urejeshaji wa mikopo, ambapo sio kila mwezi, bali itakuwa ni kila msimu wa mavuno.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment