Image
Image

Kwa kazi hii,NEC inastahili pongezi.

JIJI la Dar es Salaam limevuka lengo la uandikishaji wapiga kura katika daftari la kudumu la wapiga kura, licha ya zoezi hilo kuanza kwa kusuasua.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katika hili, inastahili pongezi kubwa. Tunasema hivyo kwa kuwa, kwa mara ya kwanza kutumika kwa mfumo mpya wa kielektroniki ujulikanao kama Biometric Voter Registration (BVR) imeweza kufanikiwa kuvuka lengo karibu kila mkoa ilipoandikisha Watanzania kwenye Daftari la Kudumu la Wapigakura.
Kwa Dar es Saalam pekee, lengo lilikuwa kuandikisha watu 2,810,423, lakini hadi kukamilika kwake, watu 2,845,256 ambao ni sawa na asilimia 101.2 walikuwa wameandikishwa.
Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu, Damian Lubuva alisema juzi katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari kuhusiana na kukamilika kwake mkoa wa Dar es Salaam kwamba hadi Agosti 4 mwaka huu, wananchi waliojiandikisha katika wilaya ya Kinondoni walikuwa 1,157,6617 sawa na asilimia 105, ambapo lengo lilikuwa 1,102,565.
Alisema wilaya ya Temeke iliandikisha wapigakura 886,564 sawa na asilimia 98.9 wakati lengo lilikuwa watu 896,142. Akasema wilaya ya Ilala imeandikisha wapigakura 886,564 sawa na asilimia 98.9 na lengo lilikuwa ni 811,716.
Tume imetangaza kukamilika rasmi kwa zoezi hilo kwa mkoa wa Dar es Salaam na hivyo kuhitimisha rasmi uandikishaji wa wapiga kura kwa kutumia mfumo wa kielektroniki wa BVR kwa nchi nzima bila kuwepo na malalamiko ya watu waliokuwa wana nia ya kujindikisha kushindwa kufanya hivyo kwa sababu zozote zile.
Wapo waliokuwa wakibeza zoezi zima, kabla halijaanza, lilipoanza mikoani hadi lilipohitimishwa Dar es Salaam, lakini Tume imefanikiwa kulipita lengo la uandikishaji. Haya ni mafanikio makubwa katika nchi changa kama hii ambayo teknolojia haijakua vya kutosha.
Tume imeweka wazi kwamba sasa kazi iliyopo ni kuliweka wazi daftari hilo la awali ambapo hadi sasa tayari mikoa 19 imekwishapelekewa. Akasema mikoa mingine ikiwemo Zanzibar na Dar es Salaam mchakato wa kuandaa daftari la awali unaendelea na unatarajiwa kukamilika muda si mrefu kuanzia sasa baada ya uandikishaji kukamilika.
Ni ya kufanya hivyo ni kutoa fursa kwa wale waliojiandikisha kuweza kusahihisha taarifa zao, kuhamisha taarifa za wapia kura waliohama kutoka kata au jimbo moja kwenda kata au jimbo lingine, kutoa kadi kwa wapiga kura waliopoteza kadi zao na kuangalia iwapo taarifa za mpiga kura aliyejiandikisha zipo kwenye daftari.
Sifa nyingine ambayo Tume imeainisha ni kuweka pingamizi kwa jina au taarifa za mpiga kura asiye na sifa ya kuwemo katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Ni ukweli ulio wazi kwamba uandikishwaji katika mkoa wa Dar es Salaam na nchi nzima umefanyika na kukamilika kwa mafanikio makubwa mbali na changamoto za hapa na pale zilizojitokeza hasa katika hatua za mwanzo za uandikishaji.
Tunaipongeza Tume hiyo kwa mafanikio haya na tunaamini Uchaguzi Mkuu ujao utafanikiwa vile vile kwa asilimia kubwa kwa maana ya kwamba watu wengi watajitokeza kupiga kura.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment