Image
Image

Tanzania yazidi kupotea Fifa.

TANZANIA imeendelea kufanya vibaya kwenye nafasi ya ubora wa viwango vya Fifa na sasa imeporomoka mpaka nafasi ya 140 kutoka 139 mwezi uliopita.
Timu ya soka ya taifa, Taifa Stars imekuwa ikifanya vibaya tangu kuanza kwa mwaka huu hali iliyofanya Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la soka Tanzania (TFF) imfute kazi kocha Mholanzi Mart Nooij na mikoba yake kupewa mzawa Charles Mkwasa.
Kwa mujibu wa viwango hivyo, timu za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati ambazo ni wanachama wa Baraza la vyama vya soka kwa ukanda huo (Cecafa) zimezidi kuwa taaban kulinganisha na timu za Kusini zinazofanya vizuri kila kukicha.
Timu zilizo chini ya Cecafa zilizo kwenye ‘ahueni’ kidogo ni Uganda inayoshika nafasi ya 74, Sudan ya 87, Rwanda ya 91, Ethiopia ya 99, Kenya ya 116 na Burundi ya 132.
Sudan Kusini ipo nafasi ya 195, Eritrea ya 203, Somalia ya 204 na Djibouti ni ya 206. Viwango hivyo vimetoka Stars ikijiandaa kumenyana na Nigeria mechi ya kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Mataifa Afrika mwaka 2017 Septemba 5 mwaka huu. Wapinzani hao wa Stars Nigeria wapo katika nafasi ya 53.
Aidha wapinzani wengine wa Stars kwenye kuwania michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 Malawi wameshika nafasi ya 98
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment