Image
Image

Yanga yasajili beki wa Togo.

YANGA imemsajili beki wa kati Vincent Baossou kutoka Togo kuziba nafasi ya Joseph Zuttah wa Ghana aliyetupiwa virago.
Tayari Bossou yuko nchini na inaonekana ameridhia kujiunga na Yanga ambayo inataka kuimarisha safu ya ulinzi iliyoonekana kupwaya katika michuano ya Kagame iliyoishia hatua ya robo fainali.
Beki huyo alianza soka lake kwenye klabu ya Maranatha FC mwaka 2006 na kudumu kwenye klabu hiyo mpaka mwaka 2009 akicheza jumla ya mechi 77 na kuifungia klabu hiyo magoli matano (5).
Alijiunga na klabu ya Etoile Sportive du Sahel, Januari 2010 kwa mkataba wa miaka miwili lakini mkataba wake ukavunjwa baada ya miezi mitatu baadaye akiwa ameichezea klabu hiyo mechi tatu tu, na karudi tena Maranatha FC Machi 18, 2010.
Mei 2011 alijiunga na klabu ya Navibank Saigon F.C ya Vietnam ambapo alicheza mechi 35 na kufanikiwa kufunga mabao matatu na kwa sasa alikuwa na mkataba na klabu ya Govang Hi FC ya Korea Kusini.
Pia Bossou alikuwepo kwenye kikosi cha Togo ambacho kilijitoa kushiriki michuano ya Mataifa ya Afrika 2010 baada ya basi la timu hiyo kushambuliwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni magaidi wakati wakielekea Angola ilipofanyika michuano hiyo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment