Image
Image

Mkwassa aita 29 safari ya Uturuki.

KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars Charles Mkwasa ameita kikosi cha wachezaji 29 kwa ajili ya kambi ya Uturuki huku wachezaji tisa wakitoka Azam.
Stars inatarajiwa kwenda kuweka kambi ya wiki mbili Uturuki kujiandaa na mechi ya kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Mataifa Afrika dhidi ya Nigeria itakayochezwa nchini Septemba 5 mwaka huu. Miongoni mwa wachezaji tisa wa Azam, yumo kinda Farid Mussa aliyefunga bao lililoipeleka timu hiyo kwenye fainali kwenye mechi dhidi ya KCCA ya Uganda.
Akitangaza kikosi hicho kitakachoingia kambini keshokutwa kocha Mkwasa, aliweka wazi kuwa wameangalia wachezaji kwenye mashindano ya Kagame, ambayo yamemalizika hivi karibuni.
“Kikosi hiki cha wachezaji 29 kitaingia kambini siku ya Jumapili katika hoteli ya Tansoma iliyopo Gerezani kwa ajili ya kambi ya wiki moja ya mazoezi kabla ya kwenda kuweka kambi ya siku kumi jijini Istanbul - Uturuki, ambapo itacheza michezo miwili ya kirafiki na timu za Taifa za Libya na Kuwait kabla ya kurejea nchini kuwavaa Nigeria,” alisema Mkwasa.
Katika kikosi hicho Mkwasa amewajumuisha wachezaji watano wanaocheza soka la kulipwa nje ya nchi ambao baadaye watajumuika kwa kambi ya kujiandaa kucheza na Nigeria, Septemba 2015 nchini Uturuki.
Wachezaji walioitwa ni magolikipa, Ally Mustafa (Yanga SC) na Aishi Manula (Azam FC), walinzi wa pembeni: Shomari Kapombe (Azam FC), Michael Aidan (Ruvu Shooting), Juma Abdul, Mwinyi Haji (Yanga SC) na Abdi Banda (Simba SC).
Walinzi wa kati; Hassan Isihaka (Simba SC), Nadir Haroub, Kelvin Yondani (Yanga SC), Viungo wakabaji: Himid Mao, Frank Domayo, Mudathir Yahya (Azam FC), Viungo washambuliaji ni Salum Telela (Yanga SC) na Said Ndemla (Simba SC).
Washambuliaji wa pembeni: Orgenes Mollel (Aspire – Senegal), Abdrahman Mbambi (Mafunzo), Deus Kaseke, Saimon Msuva (Yanga SC), Ramdhani Singano, Farid Musa (Azam FC), huku washambuliaji wa kati wakiwa ni John Bocco, Ame Ally (Azam FC) na Rashid Mandawa (Mwadui FC).
Wachezaji wa kimataifa waliojumuishwa katika kikosi hicho ambacho Agosti 23 kitaelekea kambini nchini Uturuki kwa kambi ya siku kumi ni Mbwana Samata, Thomas Ulimwengu (TP Mazembe – DR Congo), Mrisho Ngasa (Free State - Afrika Kusini) na Hassan Sembi (Santos FC – Afrika Kusini) na Adi Yussuf (Mansfield Town – Uingereza.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment