Image
Image

Mwalimu wa shule ya msingi atiwa mbaroni na polisi kwa madai ya ubakaji nchini China.


Mwalimu mmoja wa shule ya msingi anayeshukiwa kubaka wanafunzi ametiwa mbaroni na polisi katika mkoa wa Yunnan ulioko kusini magharibi mwa China.

Mwalimu huyo anayefunza katika shule ya msingi ya Mohei iliyoko mjini Zhaotong, alikamatwa na polisi baada ya kuripotiwa na wakazi wa eneo hilo.

Mnamo tarehe 29 mwezi Julai, polisi walifikishiwa mashtaka na mmoja wa wakazi wa mji alitoa madai ya kubakwa kwa binti yake na mwalimu huyo wa shule.

Taarifa hiyo ilizua utata kwa wakazi wa mji na kudai kwamba mwalimu huyo alitekeleza kitendo hicho kichafu kwa wanafunzi wengi wa kike wanaosoma katika shule hiyo.

Wengi wa wanafunzi waliokumbwa nam kasa huo wanasemekana kuishi majumbani mwao na jamaa wao wa karibu huku wazazi wao wakiishi na kufanya kazi katika miji mikubwa nchini China.

Uchunguzi kuhusiana na kesi hiyo bado unaendelea kufanyika nchini humo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment