Rais
wa chama cha madaktari bingwa wa figo Tanzania Dk. Onesmo Kisanga ameyasema
hayo wakati wa mkutano mkuu wa pili wa mwaka wa chama hicho unaofanyika jijini
Mwanza kwa lengo la kujadili magonjwa ya figo yanayojitokeza kwa wananchi,
namna ya matibabu ya ugonjwa huo kwa kutumia teknolojia ndogo iliyopo kama nchi
inayoendelea na kuwasilisha mrejesho juu ya tafiti mbalimbali zinazohusiana na
magonjwa ya figo.
Naye
mkurugenzi mkuu wa hospitali ya rufaa Bugando,mwanza Prof. Kien Mteta amesema
utafiti uliofanywa na daktari bingwa wa magonjwa ya figo na kisukari
Dk.Mubaraka Janmohammed mwaka 2011 na 2012, kwa wagonjwa wa kisukari katika
hospitali ya rufaa Bugando ulionyesha kuwa zaidi ya asilimia 80 ya wagonjwa hao
waliohudhuria kwenye kliniki ya hospitali hiyo walikuwa na madhara ya
ugonjwa wa figo.
Awali
akifungua mkutano huo unaofanyika kwa siku mbili,mkuu wa mkoa wa Mwanza Magesa
Mulongo amewashauri wananchi kupima afya zao mara kwa mara na kuepuka kutumia
dawa za miti shamba kwa madai kwamba zikitumika bila uangaifu zinaweza
kusababisha madhara kwenye figo, magonjwa mengine yanayoweza kusababisha
ugonjwa wa figo ni shinikizo la damu, ugonjwa wa kisukari na Ukimwi.
0 comments:
Post a Comment