Image
Image

Taasisi za fedha zashindwa kuwakopesha mikopo wazee kutokana na umri wao.


Kwa miaka mingi taasisi mbalimbali za fedha zinashindwa kutoa mikopo kwa wazee kwa madai kwamba wazee ni kundi ambalo halikopesheki kutokana na umri wao kuwa mkubwa.
Hali hiyo imeelezwa kuwa ndiyo sababu kubwa inayochangia pia Tanzania kuwa na wazee wengi masikini.
Katika kikao kilichoshirikisha wazee,wafanyabiashara,taasisi za fedha na serikali kutoka wilaya sita za Mkoa wa Njombe, ajenda kubwa ni kutafuta ufumbuzi wa kuhakikisha wazee wanatambuliwa na taasisi za fedha na kukopesheka.
Shirika linalohudumia wazee la Padi Tanzania, kwa miaka 15 limekuwa likifanya kazi ya kuwakopesha wazee katika mikoa ya Ruvuma na Njombe, na limetoa vyeti vya usajili kwa vikundi 24 vyenye wazee 1,500 Mkoani Njombe,  lengo likiwa ni kuendelea kufungua mianya ya taasisi za fedha na wafanyabiashara kuwatambua wazee na kuwapa mikopo.
Kwa upande wao wazee wa Njombe wanasema ifike wakati fikra za kwamba wazee hawakopesheki zikome, na kwamba wapo tayari kukopa na ni warejeshaji wazuri wa mikopo kuliko inavyofikirika na vyombo vingi vya fedha kuwa wamefikia ukomo wa kuishi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment