Image
Image

News Alert:MPINGA - Awaagiza watendaji wake kutoa Elimu ya usalama barabarani kwa waendesha BODABODA.


Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani katika Jeshi la Pilisi Tanzania Naibu Kamishna wa Polisi MOHAMMED MPINGA amewaagiza watendaji wa jeshi hilo kutoa elimu ya usalama barabarani kwa waendesha pikipiki zinazobeba abiria kufuatia kuongezeka kwa pikipiki hizo
Kamishna wa Polisi MOHAMMED MPINGA ametoa agizo hilo wakati akizungumza na waendesha pikipiki hizo maarufu kama boda boda wa jiji la Tanga wakati wa ufungaji wa mafunzo ya elimu ya usalama barabarani kwa ajili ya kupunguza ajali ambazo zimekuwa zikipoteza maisha ya Watanzania kwa sababu ya kushindwa kuzingatia sheria za usalama barabarani
Kwa upande wake, Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani Tanga Mrakibu Mwandamizi wa Polisi ABDI ISSANGO amesema katika kipindi cha kuanzia mwaka 2014 hadi sasa jeshi hilo limeshatoa mafunzo kwa waendesha pikipiki zaidi ya 340 katika jiji la Tanga, idadi ambayo ni kubwa na imesaidia kupunguza ajali za barabarani
Naye Ofisa Habari waKkampuni ya Bia Tanzania ambayo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Tanzania iliratibu zoezi la utoaji wa elimu ya usalama barabarani kwa waendesha pikipiki za BODABODA DORISI MALULU amewataka wasafirishaji wa pikipiki kuwa mabalozi wazuri kwa wenzao ambao hawajapata elimu hiyo, ili waweze kunufaika.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment