Image
Image

Breaking News:UKAWA na jeshi la polisi wavutana juu ya namna kumsindikiza mgombea urais chadema kuchukua fomu NEC.


Jeshi la polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam na Umoja wa katiba ya wananchi UKAWA umeonekana kuvutana na kuwa na majibu tofauti juu ya namna ya Kusindikizwa mgombea urais wa CHADEMA kupitia UKAWA  kwenda NEC mapema leo.
Kupitia taarifa ya kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova amesema kuwa  maandamano ya kusindikizwa mgombea urais wa CHADEMA yana kibali cha kuanzia makao makuu ya kinondoni ilipo CHADEMA hadi NEC na kurudi,lakini sikama inavyoelezwa kuwa maandamano hayo yataanzia Ofisi za CUF ilala buguruni na kupitia NCCR hivyo kwenda NEC kuchukua fomu suala hilo hawalitambui na hawalijui kwani huenda likasababisha fujo na mzunguko usio wa lazima na kuweka foleni maeneo ya Dar es Salaam na viunga vyake.

Katika kuliweka sawa suala hili moja kwa moja tulimtafuta mwenyekiti mwenza wa UKAWA ambaye pia ni mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe kufafanua hili ambapo amesema kuwa wao hawana taarifa yeyote ya mabadiliko ya kumsindikiza mgombea urais wa chama chao kwenda kuchukua fomu ofisi za NEC leo hii.
Pia Mh.Mbowe ameongeza kwa kusema kuwa dhamira yao ya kumsindikiza mgombea urais kupitia CHADEMA na UKAWA kiujumla ipo palepale kwani suala la kuanzia CUF ama NCCR sijambo la kushangaa kwa kuwa sehemu hizo zote ni umoja wao ndani ya UKAWA.
Taarifa ya jeshi la Polisi,kukubali maandamano.
 Jeshi la polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam limeona ni Busara kuruhusu maandamano ya wafuasi wa UKAWA kumsindikiza mgombea wao ili kuleta mahusiano mazuri kati ya Vyama hivyo na Jeshi la Polisi. Jeshi la polisi litasindikiza maandamano hayo. Aidha kamanda Kova amesema hayo si maandamo bali ni usindikizaji wa mgombea huyo wa UKAWA.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment