Image
Image

Twiga Stars kuingia kambini Zanzibar leo.

TIMU ya Taifa Tanzania ya Wanawake (Twiga Stars) inatarajiwa kuingia kambini leo kisiwani Zanzibar kujiandaa na Michezo ya Afrika (All Africa Games) itakayofanyika mwezi ujao nchini Congo Brazzaville.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto alisema kuwa kikosi hicho kitakuwa na wachezaji 25 chini ya kocha wao mkuu, Rogasian Kaijage. Alisema kuwa kikosi kinaendelea na mazoezi kujiandaa na michezo hiyo, ambapo Tanzania ilikata tiketi ya kushiriki fainali hizo baada ya kuiondoa Zambia kwa kuifunga jumla ya mabao 6-5.
Awali, timu hiyo ilikuwa imepiga kambi Mbande huku wenzao wa Taifa Stars wakitafutiwa kambi nje ya nchi kwa ajili ya maandalizi ya mchezo dhidi ya Nigeria utakaofanyika baadae mwezi ujao.
Taifa Stars iko katika kampeni za kufuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) zitakazofanyika Gabon 2017 na tayari imeshafungwa na Misri katika hatua ya makundi. Kizuguto alisema Twiga Stars inaingia kambini kwa gharama za TFF, huku jitihada za TFF kuwasiliana na Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) zikiendelea kuona ni jinsi gani kamati hiyo inaihudumia timu hiyo ya Taifa kwa ajili ya maandalizi ya michuano hiyo.
TFF inatambua kuwa TOC ndio wana jukumu la kuhudumia timu za Taifa kuelekea kwenye michuano hiyo ya Michezo ya Afrika, ikiwemo Twiga Stars. Twiga Stars ambayo imefuzu kwa fainali za Michezo ya Afrika itakayoanza kutimua vumbi Septemba 04 – 17 imepangwa kundi A pamoja na wenyeji Congo Brazaville, Nigeria pamoja na Ivory Coast.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment