Image
Image

Utapiamlo na udumavu wa afya kwa watoto wazidi kushika kasi Shinyanga.


Mkoa wa Shinyanga umebainika una idadi kubwa ya watoto wenye udumavu wa afya na utapiamlo hali inayosababishwa na ukosefu wa elimu ya afya ya uzazi kwa wananchi wa mkoa huo na Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kuwa asilimia thelathini ya watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano wamedumaa.

Hayo yamesemwa na katibu tawala wa wilaya ya kishapu Bw.Shadrack Kengese kwa niaba ya mkuu wa mkoa washinyanga katika maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji duniani yaliyofanyika kimkoa katika kata ya ukenyenge wilaya ya Kishapu huku akiwataka wanawake kujenga tabia ya kunyonyesha watoto wao hadi kufikia umri wa miaka miwili na kuendelea ili kujenga familia yenye nguvu na isiyosumbuuliwa na maradhi.

Afisa mahusiano wa shirika la SAVE THE CHILDREN mkoa wa Shinyanga Bw. Petro Mahui amesema lengo la maadhimisho hayo ni kuhakikisha jamii nzima inaweka mikakati ya kushiriki kikamilifu katika kupiga vita utapiamlo na udumavu wa afya kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano hali itakayoliwezesha taifa kukua kiuchumi na kufikia malengo ya milenia.

Kwa upande wake afisa mwezeshaji taasisi ya chakula na lishe mkoa wa shinyanga Bi.Debora Charwe amewataka wadau wa afya nchini kuhakikisha elimu ya unyonyeshaji kwa kipindi kinachoshauriwa inawafikia walengwa wote huku akiwataka waajiri kutoa nafasi maalum kwa waajiriwa wanawake wanaonyonyesha kuendelea kufanya hivyo mahala pa kazi kama sheria inavyoelekeza.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment